Jinsi ya kuunlock E173u-1 Airtel Tanzania itumie mitandao yote
Hii ni modem ya Huawei E173u-1 Airtel ambayo inatumia SIM Card wa Airtel Tanzania tu kwahiyo ukiweka SIM card ya mtandao mwingine inakuandikia Invalid SIM Card
Kwa kutumia njia hii utaweza kuunlock modem yako ya E173u-1 Airtel Tanzania na utaweza kutumia SIM Card ya mtandao wowote ule unaoutaka
Muhimu
- Hakikisha hakuna kifaa kingine kimechomekwa kwenye computer isipokuwa modem yako.
- Hakikisha computer yako ina charge 50% na kuendelea
- Usitumie Unlocked firmware tofauti na hii uta-brick modem yako. Itakufa jumla
- Usizime computer yako kipindi cha kurun unlocked firmware
- Usichomoe modem yako kipindi cha kurun unlocked firmware
- Soma kwanza maelezo kabla ya kuunlock modem yako
- Hatua moja ni muhimu sana, ukiruka hatua moja basi hatua nyingine haitafanya kazi
Namna ya kuunlock Huawei E173u-1 Airtel Tanzania
1. Weka SIM Card ya mtandao mwingine kisha chomeka modem yako kwenye computer
2. Install dashboard ya modem yako ili kuinstall drivers za modem yako
3. Baada ya kuinstall, itafunguka dashboard ya modem yako. Ifunge
4. Soma maelezo yaliyopo kwenye PDF kwenye File
Hongera! Mpaka hapa utakuwa umefanikiwa kuunlock E173u-1 Airtel Tanzania na utaweza kutumia SIM Card ya mtandao wowote ule unaoutaka.
Utatakiwa kutengeneza APN (Internet Setting kwa hasa SIM Card ya Halotel)
Bonyeza Tools kwenye dashboard ya modem yako
Bonyeza kwenye Options
Bonyeza kwennye Profile Management
Bonyeza New
Kwenye Profile Name: Andika jina lolote
APN: Static, andika Internet kisha bonyeza Save (1) na bonyeza Ok (2)
Mpaka hapa, utakuwa umeweza kutengeneza new profile
Enjoy!
Post a Comment