Namna ya kuunlock E303h-1 Tigo Tanzania itumie mitandao yote
Hii ni modem ya Tigo E303h-1 ambayo inatumia SIM Card ya mtandao mmoja tu na ukiweka laini ya mtandao mwingine inakuandikia invalid SIM Card.
Kwa kutumia njia hii utaweza kuunlock modem ya Tigo Tanzania E303H-1 na utaweza kutumia SIM Card ya mtandao wowote ule unaoutaka
Muhimu
- Hakikisha hakuna kifaa kingine kimechomekwa kwenye computer isipokuwa modem.
- Hakikisha computer yako ina charge 50% na kuendelea
- Usitumie Unlocked firmware tofauti na hizi uta-brick modem yako. Itakufa jumla
- Usizime computer yako kipindi cha kurun unlocked firmware
- Usichomoe modem yako kipindi cha kurun unlocked firmware
- Soma kwanza maelezo kabla ya kuunlock modem yako
- Hatua moja ni muhimu sana, ukiruka hatua moja basi hatua nyingine haitafanya kazi
Jinsi ya kuunlock Huawei E303h-1 Tigo Tanzania itumie mitandao yote
1. Chomeka modem yako kwenye computer, itajitokeza dashboard ya Tigo, ifunge. Hakikisha modem yako ina laini ya mtandao mwingine au haina kabisa
2. Run Huawei code calculator. Bonyeza kwenye Huawei tab>>>>> weka IMEI kisha bonyeza Calculate button kupata flash code
3. Run Huawei E303H-1 Tigo Tanzania unlocked firmware. Itakuomba password, weka za flash code kisha bonyeza OK
4. Iache mpaka imalize kisha bonyeza Finish
Hongera! Mpaka hapa utakuwa umeweza kuunlock modem yako ya Huawei E303H-1 na utaweza kutumia laini ya mtandao wowote ule unaoutaka.
Post a Comment